Eastern Arc Mountains Information Source
News    |    Directory    |    Library    |    Map    |    Projects/Partners   |    Links

Wadudu Waharibifu Leucaena psyllid

Gerry D. Hertel, USDA Forest Service - Forest Health and Management

1998. The Entomology and Forest Resources Digital Information Work Group, College of Agricultural and Environmental Sciences and Warnell School of Forest Resources, The University of Georgia, Tifton, Georgia 31793 U.S.A.  BUGWOOD 98-201

Wadudu waharibifu wanaoshambulia miti aina ya leucaena waitwao leucaena psyllid wamo katika kundi la wadudu lijulikanalo na wengi kama chawa wanaorukaruka wapatikanao katika mimea.  Asili yake ni Amerika ya Kati na Amerika Kusini, chimbuko la miti ya leucaena.  Mdudu huyo hata akiwa mkubwa hawezi kuonekana kwa macho.  Ana urefu wa karibu milimita mbili na rangi ya manjano.   Hutaga mayai katikati ya majani yanayochipuka kwenye ncha ya mti.  Mayai huchukua muda wa kati ya siku 10 na 12 kuwa funza, viluwiluwi na hatimaye mdudu aliyekomaa.
Mdudu huyo hupatikana sana kwenye miti michanga ya leucaena ambapo mayai, viluwiluwi wasio na mabawa na wadudu waliokomaa wenye mabawa hupatikana kwa pamoja.  Barani Afrika, mdudu huyo hupatikana katika maeneo ambapo miti aina ya leucaena hukuzwa, hasa katika Burundi, Ethiopia, Kenya, Malawi, Mauritius, Msumbiji, Reunion, Tanzania, Uganda na Zambia.

Jamii ya miti ya leucaena ina aina karibu 10 tofauti za mmea huo.  Ni mti ambao una matumizi mengi.  Ingawa njia thabiti kukabiliana na mdudu huyo mharibifu haijapatikana, wakulima na watu wenginc waliopanda leucaena hawafai kuing'oa kwa sababu kinga kamili inatafutwa bado. Wadudu wawezao kumla mdudu huyo anayeharibu leucaena wanatathminiwa.  Kadhalika, aina ya miti ya leucaena isiyoweza kuharibiwa na wadudu hao inachunguzwa.  Ye yote anayegundua kwamba mdudu huyo amerahibu mimea hiyo anaweza kuripoti na atasaidiwa ipasavyo akiwasiliana na:

Kwa sababu si rahisi kumwona mdudu huyo kwa macho, hudhihirika yupo madhara aliyoyasababisha mitini yakianza kuonekana.  Wadudu waliokomaa pamoja na viluwiluwi hudhuru miti ya leucaena kwa kufyonza utomvu kutoka kwa miti na matawi yanayochipuka, majani na maua.
Matokeo yake huwa ni kudhoofika na kukwajuka kwa majani.  Kwa kawaida, majani kwenye mimea inayochipuka yakivamiwa, huharibiwa kabisa.  Wakati mwingine, wadudu hao husababisha kukauka kabisa kwa mmea wanaouvamia. 

Wadudu wanaoharibu leucaena
Mayai ya leucaena psyllid yakiwa mtini
Mti ulio na leucaena psyllid Ramani inayoonyesha jinsi leucaena psyllid walivyoenea kutoka Amerika Kaskazini hadi Afrika kutoka 1984 hadi 1992

Maelezo yametayarishwa na Gerry Hertel wa USDA Forest Service, yametolewa na Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) na kuchapishwa na Forest Health Management Centre SLP 30241 Nairobi

Photo Credits: W. Nagamine, FAO Archives and W. M. Ciesla

line
University of Georgia The Bugwood Network Forestry Images   The Bugwood Network - The University of Georgia
College of Agricultural and Environmental Sciences and Warnell School of Forest Resources
Copyright 2004. All rights reserved.       Page last modified: Wednesday, August 8, 2001
Questions and/or comments to: bugwood@arches.uga.edu